PICHA ZA UKWELI

OMMY DIMPOZ APATA SHAVU MTV NA TRACE…!!



BAADA ya ngoma yake ya ‘Nai Nai’, kushika vilivyo msanii wa kibao hicho Omary Faraji Nyembo maarufu kama Ommy Dimpoz, ameuambia mtandao wa DarTalk kuwa amepewa mkataba na vituo vikubwa vya muziki Afrika MTV pamoja Trace ili wimbo wake uweze kupigwa kwenye vituo hivyo.

Kauli ya msanii huyo imekuja baada ya mwandsihi wa mtandao huo, kutaka kujua ni mafanikio gani aliyoyapata baada ya kibao hicho ambacho kwa namna moja amna nyingine ndicho kilichomfanya aweze kujulikana.




Dimpoz stejini


Alisema kuwa mafanikio makubwa ni kwamba kimemfanya aweze kuishi kivyake na kujitengemea kwa kila kitu, kwani awali alikuwa akiishi nyumbani.


Hata hivyo alisema kuwa mbali na mafanikio hayo lakini kimeweza kumpatia mkataba mkubwa na vituo hivyo vikubwa vya muziki Afrika kwani kwa sasa kibao hicho kinapigwa mara zote kwenye televisheni hizo.


“Nahitaji kufika mbali zaidi katika muziki wangu hivyo nafarajika kuona wimbo wangu unapigwa kwenye televisheni hizo, kwani huo ni mwanzo mzuri wa mimi kuonekana kimataifa zaidi,”
alisema Dimpoz kwa pozi.

No comments: