Meja
  Jenerali  Wynjones Kisamba, Naibu Kamanda wa Vikosi  vya  kulinda 
amani  katika Jimbo la Darfur akibadilishana mawazo na baadhi ya  
maafisa wa  Ubalozi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, katika  
mazungumzo  yake na  maafisa hao, Meja Jeneral amezungumza kwa kina  
fursa za uwekezaji  zilizopo  katika nchi  ya Sudani ya Kusini namna  
gani Tanzania na  watanzania  kama wakijipanga na wakithubutu  
watakavyoweza kunufaika na  fursa hizo ambazo amesema kwa sasa  
zimechangamkiwa sana na majirani zetu  ili hali Tanzania bado  
tukisuasua. Akazungumzia pia kuhusu operesheni  ya kulinda amani huko  
darfur na changamoto zake, lakini pia  uwepo wa  fursa ya Tanzania  
kupanua ushiriki  wake katika eneo hilo.
Baadhi
  ya Maafisa wa Ubalozi wakiwa  katika picha ya pamoja na  Meja Jenerali
  Kisamba, ambapopia alitumia mazungumzo yake na maafisa hao  
kuwashukuru  na kwa kazi nzuri ya kuiwakilisha Tanzania katika Umoja wa 
Mataifa, huku  akiwataka kuto legeza kamba katika kutetea maslahi ya 
nchi na vile vile  kutoa ushauri endelevu katika masuala mbaliambali 
yanayohusika na  utekelezaji wa majukumu yao. 
--
Na Mwandishi Maalum
Ushauri
   umetolewa kwa Tanzania na Watanzania kuamka na  kuchangamkia fursa za
  uwekezaji na biashara ambazo zimejitokeza  nchini  Sudani ya Kusini.
Ushauri
  huo umetolewa siku ya Jumatano na Meja Jenerali Wynjones Kisamba,    
Naibu Kamanda wa vikosi  vya kulinda amani  katika jimbo la Darfur    
maarufu kama UNAMID,   wakati alipokutana na kubadilishana mawazo na  
maafisa wa Ubalozi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, New York.
Meja
  Jenerali Kisamba  yuko hapa Umoja wa Mataifa, kwa ziara ya kikazi na  
mafunzo  ya maafisa wa ngazi  za juu katika misheni za Umoja wa Mataifa,
  mafunzo ambayo yameandaliwa na Idara ya Operesheni za Ulinzi wa  Amani
  ya Umoja wa Mataifa (DPKO).
“
  Tanzania tuna kila sababu ya kuwekeza nchini Sudani ya Kusini, zipo  
fursa nyingi mno kuanzia upelekaji wa chakula hadi ujenzi. Nilikuwa  
nyumbani hivi karibuni, nimekutana na viongozi mbalimbali na kuwaelezea 
 juu ya fursa hizi”. Akasema Meja Jenerali
Na
  kuongeza.” Lakini wasiwasi wangu ni kwamba tunachelewa wakati majirani
  zetu wamekwisha zichangamkia fursa hizo na wako mbali sana sasa, kwa  
 maneno mengine naweza kusema wameishaingia mpaka jikoni” alisema Meja  
Jenerali huyo kwa hisia kubwa.
Aidha
  katika mazungumzo yake na maafisa wa ubalozi,  Naibu Kamanda wa vikozi
  vya UNAMID  amebainisha kwamba kama kweli serikali, kwa kushirikiana 
na   sekta za umma na binafsi zikiamua kuingia kibiashara   Sudani ya   
Kusini hakuna tutakachopoteza.
“Sudani
  ya Kusini ndio kwanza wanaanza kuijenga nchi yao, wanachangamoto  
nyingi, sisi tunaweza kuwasaidia kwa maana ya kuwekeza na kwa kufanya  
biashara. Kwa mfano wale wanakula sana chapati,  hawana ngano, tunaweza 
 kuwauzia ngano, wanahitaji mafuta ya kupikia tunayo alizeti,  
wanahitaji  vifaa vya ujenzi, tuna viwanda vya saruji na nondo pia, kwa 
kweli fursa  zipo tunachotakiwa ni kujipanga tu na kuwahamasisha 
wafanyabiashara  wetu. Lakini kubwa na la msingi  zaidi, lazima 
Watanzania  tukubali   kuthubutu”. Amesisitiza Meja Jenerali Kisamba.
Akielezea
  kuhusu suala zima la operesheni za kulinda amani   huko Darfur,   eneo
  ambalo yeye ni Naibu Kamanda akiongoza bataliani 17 zenye wanajeshi  
wapatao17,364 wakiwamo polisi 5,511 kutoka nchi 52,  Jenerali huyo  
alisema kuwa, kama ilivyo katika fursa za uwekezaji, Tanzania pia bado  
inayo fursa kubwa ya kujiimarisha zaidi katika eneo la ulinzi wa amani.
Akaeleza
  kwamba, wanajeshi  kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) pamoja 
 na askari polisi wanaohudumu katika jimbo la Darfur wameonesha uhodari 
 wa hali ya juu kiasi cha kupigiwa mfano na mataifa mengi makubwa.
“
  Siyo kama najisifu, lakini watu wetu wameonesha uhodari na maarifa ya 
 hali ya juu, wanafanya kazi nzuri, wanaheshimika,  wananidhamu,  
wanaitangaza vema Tanzania” akasema
Na
  kusisitiza. “Tumekuwa tukizungumzwa vizuri sana na baadhi wa washirika
  wetu kama vile Norway na  Sweden. Na hii inatupatia fursa ya kujipanga
  vizuri zaidi kwa maana ya kuwaandaa na kuongeza idadi ya wanajeshi na 
 askari polisi katika eneo hilo”, akabainisha Jenerali Kisamba.
Kwa mfano, akasema licha ya mahitaji makubwa ya wanajeshi, lakini kuna hitajio kubwa la askari polisi na hasa wanawake.
“
  Tunahitaji  kuwekeza katika raslimali watu  kwa maana ya wanajeshi 
wetu  na  polisi wetu. Wanajeshi wetu ni wazuri mno, na polisi wetu ni 
wazuri  pia, lakini,  na hasa kwa   polisi wetu na kwa kuwa ndo wameanza
  karibuni. Hawa wanahitaji mafunzo zaidi katika ngazi ya kimataifa  
kutokana na ukweli kwamba mafunzo wanayopewa ni yale ya kukidhi mahitaji
  ya ndani ya nchi. Lakini ni kundi linahohitajika sana hivi sasa katika
   operesheni za kulinda amani”. akasema
Aidha
  kwa kulitambua hilo, ameeleza kwamba michakato mbalimbali inafanyika, 
 ambayo pamoja  na mambo mengine, inahusisha kuwajengea uwezo na maarifa
  wanajeshi na polisi ili waweze kukidhi mahitaji na viwango vya  
kimataifa. Jambo litakalo rahisisha uwapo  na utayari   raslimali watu  
tayari kuhudu katika operesheni za kulinda amani  mara tu tunapoombwa na
  jumuia ya kimataifa kufanya hivyo.
Akizungumizia
  hali ilivyo  katika jimbo hilo la Darfur na maeneo mengine kwa ujumla,
  Meja Jenerali Kisamba amesema  kuwa, ingawa  wanajeshi wa kulinda 
amani  wanajitahidi sana kutekeleza majukumu yao,   lakini  kusema ule 
ukweli  hadi sasa hakuna amani ya kulinda jimboni Darfur.
Hata
  hivyo, akasema wanajeshi na polisi waliopo katika eneo hilo 
wanaendelea  kutekeleza majukumu yao, yakiwemo yale ya kulinda raia, 
jukumu ambalo  linabaki kuwa kati ya majukumu makubwa kabisa ya UNAMID.
Kwa
  upande wake, Tanzania kwa sasa inacho kikosi kimoja cha kijeshi,  
kombania moja ya wahandisi wa medani, waangalizi wa amani na maafisa  
wanadhimu pamoja na polisi washauri. Ambao idadi yao yote kwa ujumla  
hadi kufikia mwezi Mei 2012 inafikia jumla 1,330.
Idadi
  hiyo inafanya nchi yetu kuwa katika nafasi ya 19 kidunia kati ya nchi 
 115 zitoazo walinzi wa amani chini ya Umoja wa Mataifa duniani. 
No comments:
Post a Comment