Rais wa CWT: Gratian Mukoba
BAADA ya mgomo wa madaktari kumalizika Taifa limeendelea kuandamwa na jinamizi la migomo hiyo baada walimu kubariki kuwepo kwa tishio la mgomo wa walimu wa shule za msingi hapa nchini limeendelea kupamba moto mkoani Iringa baada ya orodha kubwa zaidi ya asilimia 90 ya walimu katika shule za Manispaa ya Iringa kubariki kuanza mgomo wao leo .
Tishio hilo la mgomo linakuja huku shule zikitarajiwa kufunguliwa siku hiyo ya jumatatu jayo Julai 9 jambo leo limebaini kuwepo kwa maandalizi makubwa ya zoezi la walimu kujiandikisha ili kushiriki mgomo siku hiyo ya kufungua shule .
Japo zoezi hilo la kujiorodhesha linaendeshwa kwa siri na walimu hao kwa ushauri kutoka chama cha walimu wilaya mkoa na Taifa katika kuunga mkono tamko na azimio la kuitisha mgomo nchi nzima lililotangazwa na Chama cha Walimu (CWT).
Katika Mkoa wa Iringa, walimu wengi wameunga mkono mgomo huo na kwamba wako tayari kugoma Jumatatu na liwalo na liwe dhidi yao.
Mgomo
huo umeitishwa na CWT ikitaka Serikali iwaongeze walimu mshahara kwa
asilimia 100, posho kwa walimu wa sayansi kufikia asilimia 55 ya
mshahara wao, walimu wa sanaa kulipwa posho ya asilimia 50 ya mshahara,
walimu wanaofanya kazi katika mazingira magumu wapewe asilimia 30 ya
mshahara wa mwezi.
Mgomo huo wa walimu unakuja wakati hali ikiwa tete kufuatia mgomo wa madaktari ambao bado haujapatiwa tiba.
Katibu wa Chama cha walimu (CWT) Manispaa ya Iringa, Peter Mvilli alinukuliwa na gazeti la kila wiki linalotolewa
mkoani Iringa la Kwanza jamii Iringa kuwa viwango vya mishahara vya
walimu vilivyopo sasa ni vidogo, vikiongozwa kwa asilimia 100 havitakuwa
mzigo kwa serikali.
A,
posho zinazodaiwa na walimu ziliwahi kulipwa katika kipindi cha utawala
wa Rais Ali Hassan Mwinyi ambapo zililipwa kila kila mwisho wa mwezi wa
kulipa mshahara.
“Mheshimiwa Mwinyi aliheshimu posho za kipindi chote cha utawala wake, lakini Rais Benjamin Mkapa aliziondoa,” alisema.
Kwa
mjibu wa Mwalimi Mvilli, Mkapa aliamua aziunganishe kwenye mshahara na
Waraka wa Serikali ulieleza hivyo, lakini kadiri siku zilivyozidi
kusonga hakuna mwalimu aliyekuta mshahara uliounganishwa na posho.
“huo
ulikuwa usanii, posho hazikuingizwa kwenye mshahara mpaka leo,”
alisisitiza.Alifafanua kuwa mgomo wa walimu unaotakiwa kufanyika nchi
nzima, umezingatia hatua zote za kisheria na tayari kwa upande wake
ameshawaelimisha walimu wa Manispaa ya Iirnga na idadi kubwa wako tayari
kuungana na wenzao nchini kugoma ili kuishinikiza serikali kuwalipa
madai yao.
“Tayari
walimu wameshaanza kupiga kura kwa ajili ya kuunga mkono au kupinga
mgomo huo unaotarajiwa kufanyika Julai 9, mwaka huu,” alieleza.
Aidha
licha ya walimu wengi katika Manispaa ya Iringa kuunga mkono mgomo huo,
baadhi ya walimu wamepinga hatua hiyo wakieleza kuwa wao hawawezi
kuigomea Serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM).
“Shule
ya Msingi Mlangali ina walimu 20, waliounga mkono ni 18 wawili
wamepinga na sababu waliyotoa ni kuwa, kuigomea CCM kwao ni dhambi,”
alisema katibu huyo.
Gazeti
hili linayo nakala ya taarifa ya maandalizi ya mgomo ambayo imeonyesha
walimu wengi wa Manispaa ya Iirnga wakiwa wameunga mkono hatua ya mgomo.
Shule za Msingi Mawelewele, Maendeleo, Kibwabwa, Viziwi, Kihesa na
Shule za Sendari Lugalo na Mlandege ndizo ambazo walimu wake wote
wameafiki kugoma.
Katika
hatua nyingine, baadhi ya wananchi waliohojiwa na gazeti hili wiki
iliyopita walisema kazi kazi ya ualimu haina maslahi kwa wahusika, kwani
wengi wanaonekana kuishi maisha ya taabu.
Rosta
Kajuni, mkazi wa Ipogolo, Manispaa ya Iirnga aliliambia gazeti hili
kuwa, maslahi wanayopata walimu hayaendani na kazi kubwa waifanyayo.
“Hii
imesababisha hata kiwango cha elimu kushuka kwa sababu walimu wamekuwa
hawafundishi vizuri. Pia mazingira yao ya kazi ni mabovu, kwa mfano hapo
Ipogolo, nyumba za walimu hazina umeme,” alisema. Mkazi mwingine wa
Manispaa, Frank Mwangosi alisema kazi ya ualimu haiendani na maslahi
yao, kwa sababu hata nyumba za kukaa hawana na wale walio nazo huwa
hazina huduma muhimu kama umeme na maji.
“
Wengine wanaishi mbali na shule lakini hawana usafiri wa kuwawezesha
kufika vituo vyao vya kazi. Ndio maana hata kasi yao ya ufundishaji huwa
iko chini,” alieleza. Tuombe Malekano, mkazi wa Manispaa, pia
alilieleza gazeti hili kuwa mishahara ambayo walimu wanalipwa haiendani
na mfumuko wa bei uliopo hivi sasa.
Taarifa
kutoka kwa walimu mbalimbali nchini zilieleza kwamba,Serikali inatakiwa
kuwaongeza mishahara na posho ifikapo Julai Mosi, kinyume chake
hawataingia madarasani kufundisha. Mbali ya nyongeza ya mishahara na
posho, walimu wengi nchini bado wanaidai serikali malimbikizo ya madai
yao mbalimbali, ambayo pia wataka walipwe ndani ya siku thelathini
ambazo zinaishia Julai 8, mwaka huu.
Kwa
sasa shule nyingi za Msingi na Sekondari nchini zitafunguliwa Julai 9,
siku ambayo walimu wamepanga mgomo. Mapema mwezi Machi mwaka huu, Kaimu
Katibu Mkuu wa CWT, Ezekiel Oluoch, alinukuliwa na vyombo vya habari
akisema walimu wataendelea kugoma na kufanya maandamano iwapo serikali
itashindwa kutekeleza ahadi za kulipa madeni yao.
Hata hivyo mgomo huo wa walimu umeanza kupokelewa tofauti na wakazi wa manispaa ya Iringa huku baadhi ya wazazi wakiunga mkono uwepo wa mgomo huo na baadhi wakipinga kwa madai kuwa kufanya hivyo kutasababisha wanafunzi waliopo darasa la saba kufeli zaidi mwaka huu
No comments:
Post a Comment