“Nilipomaliza kuimba nikawa nimechili sehemu napumzika, lakini baada ya party kuisha nianza kukusanya vitu vyangu na baadae nikagundua kuwa kamera yangu haipo, kwa kweli nilichanganyikiwa kwa kuwa bado ni mpya kabisa na niliinunua kiasi cha dola 800 za Marekani” alisema Timbulo
Akiendelea zaidi timbulo amesema kuwa juhudi za kumsaka mtu aliyesepa na kamera hiyo ya kisa bado zinaendelea kwa kuwa sehemu kubwa ya watu waliofika siku hiyo wanafahamiana hivyo anaamini ndani ya siku chache zijazo atakuwa ameipata.
katika shoo hiyo Timbulo amerifu kuwa jukwaa alilokuwa analitumia kuwaburudisha mashabiki wake lilishindwa kuhimili vishondo na kuvunjika kufuatia watu kushindwa kuvumilia na kupanda juu alipokuwa yeye na hatimaye jukwaa hilo likasalimu amri.
No comments:
Post a Comment