Mwananchi wa kijiji cha Mzuri Makunduchi Bakari Ubwa, akitoa maoni yake
 mbele ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba, ametaka kuwe na Serekali mbili 
ya Zanzibar na Tanzania Bara na kila Serekali iwe na uwezo wake na Rais 
wa Zanzibar awe na uwezo wa kuamua mambo yake kwa ajili ya Zanzibar,Rais
 wa Zanzibar awe na uwezo wa kuchagua Mabalozi kwa ajili ya Zanzibar na 
Rais wa Tanzania pia na yeye achaguwe mabalozi wa Tanzania. 
 Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Balozi Salim Ahmed Salim, 
akizungumza kuhusiana na utoaji wa maoni ya Mabadiliko ya Katiba ya 
Tanzania katika mkutano huo uliofanyika viwanja vya Mtende. 
 Mwenyekiti wa Mkutano wa kutowa maoni ya Mabadiliko ya Katiba ya 
Tanzania Mohammed Yussuf Mshamba, akisoma vipengele wakati wa kutowa 
maoni ya mabadiliko ya katiba katika viwanja vya Mtende Makunduchi. 
  Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Tanzania Dk Mvungi, akitowa 
maelezo  kwa Wananchi wa Kijiji cha Mtende waliofika kutoa maoni yao 
katika viwanja vya Skuli ya Mtende. 
 Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Tanzania wakifuatilia maoni ya 
Wananchi wa Kijiji cha Mzuri wakiyatowa mbele ya Tume hiyo ilioanza kazi
 yake jana katika Wilaya ya Kusini Unguja Makunduchi Mkoa wa Kusini 
Unguja.
 Mwananchi wa Kijiji cha Mzuri Makunduchi akikabidhi barua yenye maoni 
yake kuhusu Mabadiliko ya Katiba, mkutano huo umefanyika katika viwanja 
vya mpira timu ya Mwenge Mzuri, 
 Mwananchi wa Kijiji cha Mtende Makunduchi Aziza Mcha, akikabidhi barua 
yake yenye maoni yake kwa Mwenyekiti wa Mkutano wa kutowa maoni ya 
mabadiliko ya Katiba ya Tanzania Mohammed Yussuf Mshamba, wakati tume 
hiyo ilipofika katika Wilaya ya Kusini Unguja kukusanya maoni ya 
Wananchi kuhusu Katiba, mkutano huo umefanyika katika viwanja vya Skuli 
ya Mtende.
 Mwananchi wa Kijiji cha Mtende Ali Khamis Ali, akichangia maoni yake kwa
 kuanza kwa historia kuhusu Mzee Karume, ambaye amesema Unguja itakuwa 
kama peponi na kweli ilikuwa hivyo kwa kujenga Nyumba za Wazee Sebleni 
na kuanzisha Viwanda mbalimbali katika Zanzibar.Amesema kuwepo kwa serikali mbili ya Zanzibar na Tanganyika na kutaka 
kuwe na Muungano wa Mkataba na kugawana sawa kwa sawa misaada 
inayopatikana.  na mambo ya muungano kugaiwa sawa. 
 Mwananchi wa Kijiji cha Mzuri Makunduchi Duli Ali Duli, akichangia maoni
 yake kwa Tume iliofika kukusanya maoni ya Wananchi kuhusu Mabadiliko ya
 Katiba ya Tanzania, amesema kuwe na Serikali mbili ya Zanzibar na 
Tanganyika, na kuondoa kasoro zilioko katika Muungano huu.
 Mwananchi wa Mtende Abuu Kombo Ramadhani, ametowa maoni yake kuwe na 
serekali mbili na kuwe na uwiano katika nafasi za Muungano kwa pande 
mbili hizi na Zanzibar iwe na rasilimali zake wenyewe bila kuingiliwa na
 upande mwengine. na bara iwe hivyohivyo.  
 Mwnchi wa Kijiji cha Mtende Mohammed Shaka Mussa, amesema nashukuru 
kuitwa Tanzania na pia Umoja ni Nguvu,Utengano ni Udhaifu. Amesema 
kuwepo na serikali mbili ya Zanzibar na Tanganyika na kila upande uwe na
 uwezo wa kuamua mambo yake na kuondoa kasoro za Muungano zilizopo ili 
kuimarisha umoja wetu. 
  Wananchi wa Kijiji cha Mzuri Makunduchi wakiwa katika viwanja vya 
Mwenge wakishiriki kutowa maoni yao wakisikiliza maoni ya Wananchi 
 mbele ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba Tanzania.iliyofika katika kijiji 
hicho kukusanya maoni ya Wananchi. 
Wananchi wa Kijiji cha Mtende wakisikiliza maoni yanayotolewa na 
Wananchi wa Mtende mbele ya Tume ya Marekebisho ya Katiba katika viwanja
 vya skuli ya Mtende 
Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Tanzania Balozi Salim Ahmed 
Salim. akibadilishana mawazo na Wazee wa Kijiji cha Mzuri 
Makunduchi Wilaya ya Kusini Unguja, baada ya kumalizika kwa utowaji wa 
maoni kwa Wananchi wa Kijiji hicho.Picha Zote na Mdau Mapara Othman-Kusini Unguja 
No comments:
Post a Comment