SERIKALI
 ya Jamhuri ya Tanzania, imelifungia gazeti la Mwanahalisi kwa muda 
usiojulikana kwakile kilichoelezwa kuwa na mwenendo wa kuandika habari 
na makala za uchozezi.
Sababu
 nyingine ya kufungiwa kwa gazeti hilo ni pamoja na kujenga uhasama na 
uzushi likiwa na nia ya kusababisha wananchi kukosa imani na vyombo vya 
dola hali inayoweza kuhatarisha amani na mshikamano wa nchi. 
Akisoma
 tamko la Serikali leo jijini Dar es salaam, Kaimu Mkurugenzi Wizara ya 
Habari (MAELEZO), Phabian Lugaikamu, alisema kuwa katika toleo la gazeti
 hilo namba 302, 303 na 304 ya mwaka 2012 na mengine yaliyotangulia 
yalichapisha habari na makala zenye kueneza na kujenga hofu kwa jamii.
“Mhariri
 wa gazeti la Mwanahalisi ameitwa na kuonywa mara nyingi lakini hataki 
kukiri kuwa maudhui ya makala zake hazina tija kwa jamii,pia hazifuati 
weledi na maadili ya taaluma ya uandishi wa habari”alisema
Aidha
 alisema kuwa mhariri huyo mara zote katika utetezi wake amekuwa 
akinukuu kifungu cha 18 cha katiba ya nchi kinachotoa uhuru wa kutoa 
maoni na kwa makusudi kutokunukuu kifungu ca 30 cha katiba hiyo 
kinachoweka ukomo wa uhuru.
“Serikali
 imeamua kulifungia gazeti hilo kutochapishwa kwa muda usiojulika kwa 
mujibu wa sheria ya magazeti ya mwaka 1976, kifungu namba 25(i),adhabu 
hiyo itaanza tarehe 30 julai,2012 kwa mujibu wa tangazo la serikali 
namba 258 lililochapishwa katika gazeti la Serikali na kutolewa jijini 
Dra es salaam julai 27,2012”alisema
chanzo:-http://sufianimafoto.blogspot.com/ 
No comments:
Post a Comment